Wanamuziki 11 Matajiri Duniani 2023

ORODHA YA WANAMUZIKI  11 MATAJIRI ZAIDI DUNIANI MWAKA 2023  

Wanamuziki matajiri duniani 2023

Muziki: Ni sanaa, saa ni ubunifu na ubunifu ni kufanya kitu ambacho wengine wanakifanya  au hawakifanyi  katika namna bora ya upekee kabisa. Katika Ulimwengu wa karne hii tuliyonayo music ni burudani na pia kazi au biashara inayotegemewa  sana na kundi kubwa la watu , wasanii, Dj's , Producers na Dancers . 

Ni wazi kubwa muziki duniani kote umebeba  mafanikio ya kundi kubwa la watu ambao wameamua kuutumikia  kama sehemu ya kazi zao. Kama ilivyo kawaida mafanikio ni zawadi kwa wale wanaojituma . Leo unasogezewa hii orodha ya wanamuziki 11 matajiri duniani mwaka 2023 . 

1. Rihanna Rihanna mwenye utajiri wa dollar 1.7 Billion , hata hivyo Rihanna mpaka kufikia mwaka 2023 ndiye msanii anaeshikilia taji  la mwanamuziki wa kike tajiri  duniani . Vyanzo vikuu vya utajiri wa Rihanna ni pamoja na biashara yake ya Cosmetics Brand ya Fenty Beauty na Brand yake ya  Savage x Fenty . 

Muziki unashika  nafasi ya tatu katika vyanzo vya utajiri wa Rihanna . Mwaka 2005-2006  hautasahaulika kamwe katika safari ya Muziki kwa mrembo huyu , Baada ya kutoa album zake mbili za awali , Music of the Sun (2005) na A Girl Like Me (2006) ambazo zote zilifanya  vizuri Billboard. Na kuanzia hapo Rihanna akawa hakamatiki  . 

2. Shawn Corey  Carter ($1.6 billion)  Shawn Corey Carter au maarufu kama Jay Z ni miongoni mwa rappers mashuhuri duniani mwenye ushawishi mkubwa na idadi kubwa sana ya wafuasi  . Ni mmiliki  wa baadhi ya vyombo vya habari na mtendaji mkuu wa record studios . Mwishoni  mwa mwaka 1980 Jay Z alianza rasmi kazi ya muziki ,  na amefanya kazi kubwa sana ya kushangaza  kwa kufanya kazi nyingi katika mfumo wa album . Ikiwemo album kama The Blueprint (2001) , The Black Album (2003) , American Gangster (2007) , na 4:44 (2017) . 

Kutokana na umahiri wake Jay Z anachukuliwa  kama kioo  katika muziki wa hip-hop na msanii asiyefananishwa  na yeyote katika muziki wa hip-hop kutokana na ushawishi mkubwa alionao . Jay ni mshindi wa tuzo za Grammy 24  huku akifunga  hesabu ya mauzo ya rekodi million 125 . Jay Z ni miongoni mwa wanamuziki matajiri duniani. Muziki ndio umemfikisha  kwenye ubilionea  .

3. Andrew Lloyd Webber ($1.3 billion ) Ni miongoni mwa wanamuziki wenye hadhi kubwa na umaarufu mkubwa katika vipindi  vyote . Andrew ni mtunzi na muandaaji wa Uingereza .  Lakini hata hivyo anaorodheshwa  kama mwanamuziki aliyefanikiwa  zaidi kibiashara  , mwaka 2001 The new York Times walichapisha zaidi juu ya habari zake . 

Andrew Lloyd Weber anazungumzwa  kama binaadamu mwenye taaluma ya ajabu sana katika muziki  huku akiwa na idadi kubwa ya tuzo alizopokea  ikiwemo knight hood ya mwaka (1992), Emmy awards , 14 Ivor Novello , Grammy Awards 3 , Olivier Awards 7 , Golden Golden Globe na nyingine nyingi. 

 4 . Sir James P Mccartney  ($1.2 billion ) Mbali na muziki ( Kuimba ) James Paul Mccartney anafahamika  kama mtunzi nyimbo na mpiga besi  katika band maarufu ya The Beatles . Anazo  tuzo ikiwemo tuzo ya The Academy , Grammy Awards 18 , ameshinda  kuingia kwenye Rock and Roll Hall Fame mara mbili . 

Lakini hata hivyo sir James Paul Mccartney amefanikiwa kufanya kazi na wasanii kama Kanye West na Michael Jackson , ni bahati aliyonayo na ujuzi wa kipekee sana .

5. Sean Combs  ($1 billion) Unamfahamu ? Maarufu kama P. Didy  ni rapper kutoka nchini Marekani , mtendaji mkuu wa record studio na mtunzi wa nyimbo pamoja na ujasiriamali . Mnamo mwaka 1990 P. Didy rasmi alianza  Kazi ya muziki na tangu kipindi hicho hakuwahi kurudi nyuma . 

Uwezo na ujuzi wake wa muziki na ujasiriamali vimemfikisha  p. Didy katika mafanikio makubwa sana . Mwaka 2002 jarida  la Fortunes lilimuorodhesha  P. Didy katika nafasi ya 12 katika 40 bora ya wajasiriamali  chini ya miaka 40 . Hata hivyo combs ni mshindi wa tuzo za Grammy 3, MTV Radio 2 na Tuzo Ya CFDA  ( Council of fashion designers of America) . 

6. Herb Alpert ($900 million)  Tangu mwaka 1960 dunia na wadau mbalimbali wa muziki walipompokea  hakuwahi kuharibu katika kazi zake . Herb Alpert amefanya  Kazi bora ambayo imempa jina na umaarufu  kila pembe ya dunia , ni hodari sana katika upigaji wa tarumbeta  . 

Hata hivyo ni mshindi wa tuzo ya Tony ,tuzo za Grammy 8 , ni msanii pekee kuwa nambari  moja kwenye billboard hot 100 Marekani akiwa kama mwimbaji na mpiga  ala , kufikia mwaka 2023 anakuwa katika orodha ya wanamuziki  11 matajiri duniani. 

7. Madonna ($850 million) Mara nyingi hujulikana  kama Malkia  wa Pop, Madonna sio tu mwimbaji au mtunzi wa nyimbo lakini mwigizaji anayejulikana pia.  Alianza  kama mpiga ngoma, mpiga gitaa   na mwimbaji katika bendi za rock za Breakfast Club, Madonna alijipatia  umaarufu kwa kutoa albamu yake ya kwanza ya Madonna mwaka wa 1983 ambayo ilishika  nafasi ya nane kwenye Billboard 200.  

Lakini hata hivyo Madonna ndiye msanii wa muziki wa kike anayeuza kazi zake   zaidi muda wote akiwa na rekodi zaidi ya milioni 300 zilizouzwa  duniani kote na pia ametengeneza  jina lake katika Waandishi 100 Wakuu  wa Wakati Wote na Wasanii   100 Wakubwa Zaidi wa Wakati Wote. Kwa miongo  minne  mfululizo, Madonna alionyeshwa  kama msanii wa kike aliyeingiza  pesa nyingi zaidi na jarida la  Forbes. 

8. Ander Romelle  Young (&850 million) Ander Romelle Young, anayejulikana zaidi kama Dk. Dre, ni mwanamuziki mashuhuri ambaye  anaweza kucheza synthesizer, mashine  ya ngoma, sampuli  na kinanda  . Yeye pia ndiye mwanzilishi  na Mkurugenzi Mtendaji wa Beats Electronics na Aftermath Entertainment. 

Akiwa yeye mwenyewe ni miongo mwa rappers na wasanii maarufu wa nyakati zote, Dr. Dre amesimamia  kazi za rappers wengine maarufu akiwemo  Eminem, 50 Cent, Snoop Dogg, Kendrick Lamar na wengine. Yeye pia ni mjasiriamali  na mfadhili na amechangia  sana katika sanaa, teknolojia na biashara.

9. Paul David Hewson ($800 million) 

Paul David Hewson, maarufu kama Bono, ni mwimbaji-mtunzi wa nyimbo, mwanaharakati na mfadhili kutoka Ireland. Mbali na muziki na uhisani , Bono pia anajulikana sana kwa ubia wake wa biashara. Yeye ndiye mwimbaji mkuu na mwimbaji mkuu wa bendi ya rock U2 na amerekodi na wasanii wengi nje ya bendi pia. 

Alijulikana sana kwa mtindo wake wa kueleza sauti na ishara kuu na maneno yake yalichochewa zaidi na uzoefu wa kibinafsi . Bono alitajwa kuwa mmoja wa Watu Bora wa Wakati wa Mwaka mnamo 2005 na alipewa taaluma ya heshima mnamo 2007 kwa huduma zake kwenye tasnia ya muziki na kwa kazi yake ya kibinadamu. 

10. Dolly Parton ($650 million)

Alizaliwa Januari 19, 1946, Dolly Parton ni mwimbaji na mtunzi  wa nyimbo anayejulikana kama mfadhili,  mwigizaji , na mfanyabiashara . Anajulikana sana kwa kazi yake ya ajabu katika muziki wa taratibu .

Alifanya albamu yake ya kwanza ya "Hello, I'm Dolly" mwaka 1967. Tayari ameuza zaidi ya rekodi milioni 100 duniani kote na yuko tayari kutoa hits zaidi katika siku zijazo.

Rekodi ya mwanamuziki wa 11 tajiri zaidi duniani 2023 inashikiliwa na Kanye West ambaye amejilimbikizia utajiri wake mkubwa kupitia muziki, mali isiyohamishika na kuidhinishwa na brand. 

11. Kanye West ($400 million)

Ni mmoja wa waimbaji tajiri zaidi duniani. Rekodi zake za muziki pekee zimeuza zaidi ya nakala milioni 160 na ndiye mshindi wa Tuzo 24 za Grammy . Yeye ni rapa ,  mtayarishaji wa rekodi, mjasiriamali, na pia mbunifu wa mitindo . 

Kufikia 2023, thamani ya Kanya West inakadiriwa karibu $ 400 milioni. Sasa akiwa na umri wa miaka 45, Kanye West ni mmoja wa wasanii wa muziki wanaouzwa zaidi duniani.  Adudwar website


Next Post Previous Post
sr7themes.eu.org