Nchini Tanzania Watumiaji Wa Simu Za Mkononi Watakiwa Kuhakiki usajili wa Sim Card Zao

NCHINI TANZANIA WATUMIAJI WA SIMU ZA MKONONI WATAKIWA KUFANYA UHAKIKI WA USAJILI WA SIM CARD ZAO . 

Uhakiki Wa Laini Za Simu Tanzania

Tanzania :
Watumiaji wa Simu Za Mkononi na sim card za mitandao mbalimbali ya simu Nchini Tanzania wanatakiwa kufanya uhakika wa usajili wa simu card zao mara moja kabla ya mwezi February . 

Mapema January 24 , Waziri wa Teknolojia ya habari na mawasiliano Nchini Tanzania Nape Nnauye amewataka wamiliki wa Simu card Nchini Tanzania kufanya uhakika wa usajili wa Sim Card kabla ya mwezi February, Aidha inaelezwa kuwa wale watakaokwenda kinyume na agizo simu card zao zitazimwa mara moja bila kuonewa huruma yeyote ile. 

Watumiaji wa Simu card Nchini Tanzania wameshauriwa kukamilisha uhakiki huo kupitia simu zao za Mkononi au kufika katika maduka ya mitandao husika ya simu Card zao wanazotumia, ikiwa ni pamoja na Tigo, Ttcl, Airtel, Vodacom na Halotel . 

Tarehe 13/2/2023 saa kumi jioni kama kutakuwa  na laini ambayo haijahakikiwa  ndio itakuwa mwisho wa kutumika  kwake,hakuna nyongeza  ya muda, wale ambao hawajahakiki  kuhakiki  ni rahisi sana unaingia  mwenyewe kwenye simu yako unahakiki  unakuwa umemaliza"_Waziri Nape Nnauye

Next Post Previous Post
sr7themes.eu.org