Watu tisa wafa 30 Kujeruhiwa ajali ya gari Katavi

Watu tisa wafa 30 Kujeruhiwa ajali ya gari wilaya Ya Tanganyika Mkoani Katavi .

Ajali ya gari Katavi

Basi la Komba's  linalofanya  Safari zake kutoka Kigoma  Mpanda Mkoa wa Katavi limepata  ajali mbaya kwenye mlima wa Nkondwe uliopo  Wilaya ya Tanganyika . 

Taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa katavi kutokana na ajali iliyotokea  Watu 9 Wamefariki dunia na wengine 30 wamejeruhiwa na majeruhi wanaendelea na matibabu kwenye hosipitali ya Majalila , Mpanda na Rufaa Katavi.  

Ajali ya gari Katavi

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Ali Makame amesema ajali hiyo ilitokea Alasiri ya Machi 6, 2023 ikihusisha basi kampuni ya Komba’s. Ameeleza kuwa baada ya kufika katika mlima huo gari liliserereka na kudondokea kwenye bonde kubwa lenye kina cha mita zisizopungua 75. 


Next Post Previous Post
sr7themes.eu.org